Wednesday, October 28, 2009

WAANDISHI WACHUKUA AKAUNTI YA BLOGGER

Anthony Komanya
Mafunzo ya Internate kwa Waandishi
Oktoba 27,2009

WAANDISHI KANDA YA ZIWA SASA 'BLOGGERS'

Imeelezwa kwamba matumizi ya Internate kupitia tovuti ya www.blogspot.com yamefanikiwa kusogeza na kuweka dunia mkononi mwa mwandishi wa habari ili atumie taarifa kama atakavyo katika wajibu wake kwa jamii.

Akitoa mada ya 'Internate inavyofanikiwa kubadili jamii duniani' Mkufunzi wa mafunzo hayo, Peik Johnsson, alifanikiwa kuthibitisha umuhimu kwa waandishi wa habri kutumia tovuti hiyo katika wajibu wao wa kuhabarisha jamii.

Alieleza kuwa kupitia tovuti hii katika Internate, mtu ataweza kuingia kwenye kurasa za website nyingine nyingi zenye manufaa makubwa katika shughuli za uandishi wa habari.

Baadhi ya website hizo ni pamoja na www.wikipedia.org (on line) ambayo ni kama kitabu cha dunia (encyclopedia) kilicho wazi kwa mtu yeyote kusoma na hata kuhariri kwa mahitaji yake ya upashanaji habari.

Wavuti hii inampa mwomba huduma ya internate fursa ya kuchagua lugha anayotaka kutumia kwani ina tafsiri za lugha nyingi kutoka kote duniani (Kiswahili kikiwemo)

Website nyingine iliyohamasisha waandishi wa habari kujiunga na akaunti ya 'blogger' ni ile ya www.ebay.com inayopatikana kwenye tofuti hiyo.

Kwa mujibu wa Johansson, 'ebay.com' ni sawa na duka la kidunia, ambamo mtu huweza kutumia kwa kununua vitu mbalimbali vikiwamo, nguo kuukuu na mpya, magari makuukuu na mapya, nyumba, kamerasiliana na bainisha kuwa kutokana na tovuti hiyo dunia yote inakuwa karibu na mwandishi mhusika wakati wowote.

Ukweli uliowazi ni kwamba, mafunzo haya yana faida kubwa na kwa mwandishi kuwa na 'blogger' ni kama kuingia katika maktaba ambamo kila kitu na taarifa anayohitaji anaweza kuipata.

Asante

No comments:

Post a Comment